Hapa Meta, tumejitolea kuwapa watu sauti na kuwahakikishia usalama.

Tangu mwaka wa 2016, tumetumia mbinu inayoitwa "ondoa, punguza, toa taarifa" kudhibiti maudhui kwenye teknolojia zote za Meta.
Hii inamaanisha tunaondoa maudhui mabaya ambayo yanaenda kinyume cha sera zetu, kupunguza usambazaji wa maudhui yenye matatizo ambayo hayakiuki sera zetu, na kuwajulisha watu kwa muktadha wa ziada ili waweze kuamua wanachofaa kubofya, kusoma au kushiriki.
Ili kusaidia katika mkakati huu, tuna sera zinazofafanua kile kinachoruhusiwa na kisichoruhusiwa kwenye teknolojia zetu. Timu zetu hufanya kazi pamoja ili kukuza sera zetu na kuzitekeleza. Inafanya kazi ifuatavyo.

1

Tunashirikiana na wataalamu wa teknolojia, usalama wa umma na haki za binadamu kutoka kote ulimwenguni kuunda na kusasisha sera zetu.

2

Tunatengeneza vipengele vya usalama, ili watu waweze kuripoti maudhui na kuzuia, kuficha au kuacha kufuata akaunti.

3

Tunatekeleza sera zetu kwa kutumia teknolojia na ukaguzi unaofanywa na watu.
Tunaweka watu salama na kuruhusu watu kutuwajibisha kwa kushiriki sera zetu, ripoti za utekelezaji na uwazi.
policy-image
Sera zetu
Sera zetu zinafafanua kile kinachoruhusiwa na kisichoruhusiwa kwenye teknolojia za Meta. Ikiwa maudhui yanakiuka sera zetu, tunachukua hatua dhidi yake.
enforcement-image
Utekelezaji wetu
Tunatumia timu za teknolojia na ukaguzi kutambua, kukagua na kuchukua hatua dhidi ya mamilioni ya vipande vya maudhui kila siku kwenye programu ya Facebook na Instagram.
transparency-reports-image
Ripoti zetu za uwazi
Tunachapisha ripoti za mara kwa mara za uwazi ili kuonyesha watu hatua tuliyopiga katika kutekeleza sera zetu.
ranking-image
Mwelekeo wetu wa kufafanua uorodheshaji
Mifumo ya akiliunde (AI) ni msingi wa uorodheshaji wa maudhui kwa matumizi mengi ya bidhaa za Meta, kama vile kuona Mipasho ya Facebook, kutazama video fupi kwenye Instagram au kuvinjari Facebook Marketplace.
Taarifa za hivi karibuni